Kulinda uhuru wa kujieleza na kuwezesha mawasiliano salama ya kimataifa kupitia teknolojia ya faragha ya chanzo wazi.

Dira Yetu

Linda uhuru wa kujieleza na wezesha mawasiliano salama ya kimataifa kupitia teknolojia ya faragha ya chanzo wazi.

Faragha Kwanza

Tukiwa na bidhaa yetu maarufu, Signal Messenger, tunaamini kuwa kutetea faragha ya mtumiaji kunamaanisha kuweka data mbali na mikono ya mtu yeyote, ikiwa ni pamoja na mikono yetu, badala ya kudhibiti data yako "kwa uwajibikaji".

Programu Huria

Kama mwanachama aliyejitolea wa jumuiya ya programu huria, tunachapisha teknolojia yetu na kushirikisha maarifa ili kuhimiza makampuni mengine kuitumia kwenye bidhaa na huduma zao wenyewe.

Isiyo ya Faida

Taasisi ya Signal ni shirika lisilo la biashara chini ya kanuni ya 501c3. Tunajivunia uteuzi huo na tuko tayari kuthibitisha kwamba shirika lisilo la faida linaweza kubuni na kuongeza ukubwa kama ambavyo biashara yoyote inayoendeshwa kwa nia ya kupata faida.

Taasisi + Kampuni

Taasisi ya Signal iliundwa mwaka wa 2018 ili kusaidia Signal Messenger ambayo ilianzishwa mwaka wa 2012. Kupitia kwa Taasisi hii, tumeweza kusaidia ukuaji wa Signal na shughuli zinazoendelea na pia kuchunguza mustakabali wa mawasiliano binafsi.

Faragha ikilinganishwa na faida

Signal ni shirika lisilo la kibiashara, lisilo na watangazaji au wawekezaji, linaloendeshwa na watu wanaoitumia na kuithamini pekee.

Kwa nini Mfumo wa Taasisi + LLC?

Tuliunda Taasisi ya Signal kama kampuni tanzu ya Signal Messenger kwa sababu tunatazamia siku moja kukuza miradi ya kuhifadhi faragha ambayo ina dhamira sawa.

Bure kwa Kila Mtu

Tunategemea msaada kutoka kwa jumuiya ili kuifanya Signal Messenger iwe programu ya bure kwa mamilioni duniani kote. Je utaiunga mkono dhamira yetu?

Wanachama wa Bodi

Picha ya Amba Kak

Amba Kak

Amba Kak ni mwanasheria na mtaalamu wa sera za teknolojia, mwenye utaalamu wa zaidi ya muongo mmoja wa katika mataifa mbalimbali akiwashauri wasimamizi wa serikali, viwanda, asasi za kiraia na uhisani. Kwa sasa ndiye Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya AI Now, shirika la utafiti wa sera linaloongoza huko New York na Mshirika Mwandamizi katika Taasisi ya Usalama wa Mtandaoni na Faragha katika Chuo Kikuu cha Northeastern University.

Amba alihudumu kama Mshauri Mkuu katika Tume ya Biashara ya Marekani ambapo alimshauri mdhibiti kuhusu masuala ibuka ya teknolojia. Kabla ya AI Now, Amba alikuwa Mshauri wa Sera ya Kimataifa huko Mozilla ambapo alianzisha na kuendeleza misimamo ya mashirika kuhusu masuala kama vile sheria za faragha za data na kutoegemea upande wowote wa mtandao katika eneo la Asia-Pasifiki na kwingineko. Kwa sasa yuko kwenye kamati ya programu ya Wakurugenzi wa Bodi kwenye Taasisi ya Mozilla. Amba alipata shahada yake ya kwanza ya BA LLB (Hons) kutoka Chuo Kikuu cha Taifa cha Sayansi ya Sheria nchini India. Ana Shahada ya Uzamili katika Sheria (BCL) na Shahada ya Uzamili katika Sayansi ya Jamii ya Mtandao kutoka Chuo Kikuu cha Oxford, ambapo alihudhuria kama Mwanazuoni wa Rhodes.

Picha ya Brian Acton

Brian Acton

Brian Acton ni mjasiriamali na mtaalamu wa programu za kompyuta ambaye alihusika kuasisi programu ya Whataspp mwaka 2009. Baada ya programu kuuzwa kwa Facebook mwaka 2014, Acton aliamua kuondoka kwenye kampuni hiyo kufuatia tofauti zilizohusisha matumizi ya data za wateja na utangazaji uliolengwa ili kuelekeza juhudi zake kwenye mashirika yasiyo ya faida. Mnamo Februari 2018, Acton aliwekeza dola milioni 50 za pesa zake ili kuanzisha Taasisi ya Signal kwa kushirikiana na Moxie Marlinspike. Taasisi ya Signal ni shirika lisilo la faida lililodhamiria kufanya kazi ya msingi kuhakikisha wanawezesha mawasiliano ya kibinafsi, yaliyo salama na yenye kupatikana kila mahali.

Kabla ya kuanzisha WhatsApp na Taasisi ya Signal, Acton alifanya kazi kama mtaalamu wa programu kwa zaidi ya miaka 25 katika kampuni kama Apple, Yahoo, na Adobe.

Picha ya Jay Sullivan

Jay Sullivan

Jay ni muunda bidhaa aliye na uzoefu mpana katika majukumu ya uongozi wa bidhaa na uhandisi wa teknolojia ya watumiaji. Hivi karibuni, alikuwa Meneja Mkuu wa bidhaa za watumiaji na mapato wa Twitter, akiongoza uhandisi, bidhaa, muundo, utafiti na sayansi ya data. Kabla ya kuwa Twitter, Jay alikuwa Facebook, ambapo aliongoza uundaji wa Mratibu wa AI wa Reality Labs' na kisha akaongoza timu za bidhaa za Faragha, Uadilifu, na Mifumo za Messenger na Instagram Direct. Jay alikuwa Makamu Mwandamizi wa Bidhaa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Uendeshaji huko Mozilla, ambapo aliongoza matoleo makubwa ya Firefox wakati wa inaanza kuinuka/kujulikana na alikuwa mshawishi wa jukwaa la wavuti na kuwapa watu chaguo na udhibiti zaidi mtandaoni.

Jay pia amekuwa mwanzilishi wa shirika changa, mwanzoni mwa maisha yake ya kikazi alikuwa mhandisi wa programu na meneja wa uhandisi hapo Firefly Network (iliyonunuliwa na Microsoft) na Oracle.

Jay ana shahada ya sayansi, B.S. katika Hisabati kutoka Chuo cha Yale na ndiye mvumbuzi mwenza wa hataza kadhaa nchini Marekani.

Picha ya Katherine Maher

Katherine Maher

Katherine Maher ni Mkurugenzi Mtendaji wa zamani na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Wikimedia, inayohusika na Wikipedia. Kwa sasa yeye ni Mshirika Mwandamizi asiye mkazi katika Baraza la Atlantiki, ambapo kazi yake inazingatia makutano ya teknolojia, haki za binadamu, na demokrasia. Kabla ya Wikimedia, alikuwa Mkurugenzi wa Utetezi wa shirika la haki za kidijitali la Access Now. Maher ni mwanachama wa muda wa Baraza la Mahusiano ya Kigeni, Kiongozi wa Jukwaa la Kiuchumi la Vijana Ulimwenguni, na mshirika wa usalama katika Mradi wa Usalama wa Kitaifa wa Truman. Yuko kwenye bodi ya wakurugenzi wa Kituo cha Teknolojia na Demokrasia, Ripoti za Watumiaji, Maktaba ya Umma ya Kidijitali ya Marekani, Wanasayansi wa Adventure, na System.com, pia ni mdhamini wa Chuo Kikuu cha Marekani cha Beirut. Ni mjumbe mteuliwa wa Bodi ya Sera ya Mambo ya Kigeni ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, ambapo anamshauri Waziri wa Mambo ya Nje kuhusu sera ya teknolojia. Alipata Shahada yake ya Kwanza katika Masomo ya Mashariki ya Kati na Kiislamu mnamo 2005 kutoka Kitivo cha Sanaa na Sayansi cha Chuo Kikuu cha New York, baada ya kusoma katika Taasisi ya Lugha ya Kiarabu ya Chuo Kikuu cha Amerika huko Cairo, Misri, na Institut français d'études de Damas (L'IFEAD) huko Damascus, Syria.

Picha ya Meredith Whittaker

Meredith Whittaker

Meredith Whittaker ni Rais wa Signal na mwanachama wa Bodi ya Wakurugenzi ya Taasisi ya Signal.

Ana uzoefu wa zaidi ya miaka 17 kwenye teknolojia, tasnia ya uhifadhi, elimu na serikali. Kabla ya kujiunga Signal kama Rais, alikuwa Profesa wa Utafiti wa Minderoo katika Chuo Kikuu cha New York, na aliwahi kuwa Mkurugenzi wa Kitivo cha Taasisi ya AI Now ambayo alishiriki kuianzisha. Utafiti na kazi zake za kitaaluma zilisaidia kuunda sera ya kimataifa ya AI na kubadilisha mtazamo wa umma kuhusu AI ili kutambua vyema mbinu za ufuatiliaji kwenye biashara na mkusanyiko wa rasilimali za viwandani ambazo AI ya kisasa inahitaji. Kabla ya Chuo Kikuu cha New York, alifanya kazi Google kwa zaidi ya muongo mmoja, ambapo aliongoza timu za bidhaa na uhandisi, alianzisha Kikundi cha Utafiti Huru cha Google, na mshiriki mwanzilishaji wa M-Lab, jukwaa la kupima mtandao linalosambazwa kimataifa ambalo sasa ni chanzo kikubwa zaidi cha data zilizo wazi duniani kuhusu utendaji kazi wa mtandao. Alisaidia katika uratibu Google. Alikuwa mmoja wa waandaaji wakuu waliokuwa wakipambana dhidi ya muitikio hafifu wa kampuni kuhusuiana na AI na madhara yake, na alikuwa mratibu mkuu wa Google Walkout. Ameishauri Ikulu ya Marekani, FCC, Jiji la New York, Bunge la Ulaya, na serikali nyingine nyingi na mashirika ya kiraia kuhusu faragha, usalama, akili unde (AI), sera ya mtandao na vipimo. Na hivi karibuni alimaliza muda kama Mshauri Mkuu wa AI kwa Mwenyekiti katika Tume ya Biashara ya Marekani.

Mstaafu wa Heshima

Picha ya Moxie Marlinspike

Moxie Marlinspike

Moxie Marlinspike ni muasisi wa Signal.